Alliance Pledge

Kwa kujiunga na “Route to Food Alliance” inamaanisha wewe ni mojawapo wa watu wanaopigania haki za chakula nchini Kenya. Sababu ya sisi kuwepo ni kuwa na ushirikiano wae fikra sawa na watu kutoka sekta mbali mbali haswa - kutoka kwa serikali, vyombo vya habari, asasi za kiraia, taaluma, wakulima na sekta za kibinafsi wanaotaka kufanya kazi kwa pamoja kukomesha njaa nchini and kutokuweko na lishe bora. Kwa hivyo;

  1. Ninatambua kuwa kuweko kwa chakula bora ni haki ya kibinaadamu inayopatikana katika kipengele cha 43 cha katiba ya Kenya¸ ambapo kila mtu, mwanamume mwanamke na mtoto ana haki ya ya kuwa huru kutokana na njaa na kuwa na chakula cha viwango halisi vinavyokubalika.
  2. Ninapinga kwa nguvu viongozi au wafanyakazi wa uma wanaotumia chakula au misaada ya chakula kisiasa.
  3. Ninaunga mkono mabadiliko ya sheria ya kijinsia kijumla ambayo inaimarisha nafasi ya wanawake – kuwa sawa na wanaume – katika sekta za kilimo, ufugaji wa wanyama na uvuvi.
  4. Naunga mkono viongozi wanaoendeleza uhuru wa chakula nchini Kenya kwa kulinda na kuwekeza katika ukulima wa viwango vya chini mashinani, mgawo na kuongeza thamani, wakizingatia kushiriki kwa wanaume kwa wanawake, wazee kwa vijana ambao wanateseka kutokana na ukosefu wa chakula wa mara kwa mara.
  5. Naelewa kuwa njaa na lishe duni ni shida ya mara kwa mara, si janga la mara moja tu ambalo linasababishwa na mabadiliko ya hali ya anga. Kwa hivyo, ninaunga mkono mipango endelevu ya pamoja kati ya wizara za serikali husika, (kama vile wizara ya elimu,maji, afya, miundo msingi, mazingira, fedha na kilimo) kama hatua muhimu katika kushughulikia shida iliyopo.
  6. Naunga mkono sheria, sera na utendakazi za uzalishaji na ulaji wa chakula ambazo zinakubalika kijamii, kimazingira na kiuchumi. Hadi sasa, ninapinga sulihisho ambazo zinatetea matumizi ya vyakula vya kisaki (GMO), mbolea isiyo asili na dawa za wadudu.
  7. Dhamira yangu kwa hii ahadi inamaanisha nitajihusisha katika mijadala kuhusu chakula na usalama wa chakula. Nitauliza maswali ya maelezo rahisi kuhusu sababu za wakenya wengi kuwa na njaa, kutoweza kumudu gharama ya chakula, au kutoweza kupata chakula salama. Nitapinga madai kuwa Kenya iko salama kwa ugao wa chakula.
  8. Nitatumia elimu yangu, ujuzi, nafasi yangu, mitandao ya kijamii na njia nyiingine zote kadri ya uwezo wangu kuchangia katika kuafikia haki ya kibinaadamu kupata chakula
* indicates required
Would you like to receive emails from the RTFI? *

We keep your information safe. You can view our Privacy Policy here.

Stories from Alliance Members

Kai Njeri

Easter Achieng

Vincent Fibanda

Nichodemus Omundo

Daniel Muteti

Chadwick Bironga

Rael Adhiambo

Edith Kemunto